2 Reubeni, na Simeoni na Lawi, na Yuda;
3 na Isakari, na Zabuloni, na Benyamini;
4 na Dani, na Naftali, na Gadi, na Asheri.
5 Na nafsi zile zote zilizotoka viunoni mwa Yakobo zilikuwa ni nafsi sabini; na huyo Yusufu alikuwa huko ndani ya Misri tangu hapo.
6 Yusufu akafa, na ndugu zake wote, na watu wote wa kizazi kile.
7 Na wana wa Israeli walikuwa na uzazi sana, na kuongezeka mno, na kuzidi kuwa wengi, nao wakaendelea na kuongezeka nguvu; na ile nchi ilikuwa imejawa na wao.
8 Basi akainuka mfalme mpya kutawala Misri, asiyemjua Yusufu.