23 Jua lilikuwa limechomoza juu ya nchi Lutu alipoingia Soari.
24 Ndipo BWANA akanyesha juu ya Sodoma na juu ya Gomora kiberiti na moto toka mbinguni kwa BWANA.
25 Akaangusha miji hiyo na Bonde lote, na wote waliokaa katika miji hiyo, na yote yaliyomea katika nchi ile.
26 Lakini mkewe Lutu akatazama nyuma yake, akawa nguzo ya chumvi.
27 Ibrahimu akatoka asubuhi kwenda mahali aliposimama mbele za BWANA,
28 naye akatazama upande wa Sodoma na Gomora na nchi yote ya hilo Bonde, akaona, na tazama, moshi wa nchi ukapanda, kama moshi wa tanuru.
29 Ikawa Mungu alipoiharibu miji ya Bondeni, Mungu akamkumbuka Ibrahimu, akamtoa Lutu katika maangamizi alipoiangamiza miji hiyo aliyokaa Lutu.