4 Basi akampa Bilha mjakazi wake kuwa mkewe. Yakobo akaingia kwake.
5 Naye Bilha akapata mimba, akamzalia Yakobo mwana.
6 Raheli akasema, Mungu amenipa haki yangu, naye amesikia sauti yangu, akanipa mwana. Kwa hiyo akamwita jina lake Dani.
7 Bilha, mjakazi wa Raheli, akapata mimba tena, akamzalia Yakobo mwana wa pili.
8 Raheli akasema, Kwa mashindano makuu nimeshindana na ndugu yangu, nikashinda. Akamwita jina lake Naftali.
9 Lea alipoona ya kuwa ameacha kuzaa, alimtwaa Zilpa, mjakazi wake, akampa Yakobo kuwa mkewe.
10 Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana.