10 Enoshi akaishi baada ya kumzaa Kenani miaka mia nane na kumi na mitano, akazaa wana, waume na wake.
11 Siku zote za Enoshi ni miaka mia kenda na mitano, akafa.
12 Kenani akaishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 Kenani akaishi baada ya kumzaa Mahalaleli miaka mia nane na arobaini, akazaa wana, waume na wake.
14 Siku zote za Kenani ni miaka mia kenda na kumi, akafa.
15 Mahalaleli akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
16 Mahalaleli akaishi baada ya kumzaa Yaredi miaka mia nane na thelathini, akazaa wana, waume na wake.