4 Siku za Adamu baada ya kumzaa Sethi zilikuwa miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.
5 Siku zote za Adamu alizoishi ni miaka mia kenda na thelathini, naye akafa.
6 Sethi akaishi miaka mia na mitano, akamzaa Enoshi.
7 Sethi akaishi baada ya kumzaa Enoshi miaka mia nane na saba, akazaa wana, waume na wake.
8 Siku zote za Sethi ni miaka mia kenda na kumi na miwili, akafa.
9 Enoshi akaishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 Enoshi akaishi baada ya kumzaa Kenani miaka mia nane na kumi na mitano, akazaa wana, waume na wake.