1 Maono yake Obadia.Ndivyo asemavyo Bwana MUNGU juu ya Edomu;Tumepata habari kwa BWANA,Na mjumbe ametumwa kati ya mataifa,Akisema, Haya, inukeni ninyi;Na tuinuke tupigane naye.
2 Tazama, nimekufanya mdogo kati ya mataifa;Umedharauliwa sana.
3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya,Wewe ukaaye katika pango za majabali,Mwenye makao yako juu sana;Asemaye moyoni, Ni nani atakayenishusha mimi?
4 Ujapopanda juu kama tai,Ijapokuwa kioto chako kimewekwa kati ya nyota,Nitakushusha kutoka huko; asema BWANA.
5 Kama wevi wangekujilia, kama wanyang’anyi wangekujilia usiku, (jinsi ulivyokatiliwa mbali!) Je! Wasingeiba kiasi cha kuwatosha? Kama wachumao zabibu wangekujilia, je! Wasingeacha baadhi ya zabibu, ziokotwe?