13 Amenichoma viunoKwa mishale ya podo lake.
14 Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote;Wimbo wao mchana kutwa.
15 Amenijaza uchungu,Amenikinaisha kwa pakanga.
16 Amenivunja meno kwa changarawe;Amenifunika majivu.
17 Umeniweka nafsi yangu mbali na amani;Nikasahau kufanikiwa.
18 Nikasema, Nguvu zangu zimepotea,Na tumaini langu kwa BWANA.
19 Kumbuka mateso yangu, na msiba wangu,Pakanga na nyongo.