22 Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii,Kwa kuwa rehema zake hazikomi.
23 Ni mpya kila siku asubuhi;Uaminifu wako ni mkuu.
24 BWANA ndiye fungu langu, husema nafsi yangu,Kwa hiyo nitamtumaini yeye.
25 BWANA ni mwema kwa hao wamngojeao,Kwa hiyo nafsi imtafutayo.
26 Ni vema mtu autarajie wokovu wa BWANANa kumngojea kwa utulivu.
27 Ni vema mwanadamu aichukue niraWakati wa ujana wake.
28 Na akae peke yake na kunyamaza kimya;Kwa sababu Bwana ameweka hayo juu yake.