26 Ni vema mtu autarajie wokovu wa BWANANa kumngojea kwa utulivu.
27 Ni vema mwanadamu aichukue niraWakati wa ujana wake.
28 Na akae peke yake na kunyamaza kimya;Kwa sababu Bwana ameweka hayo juu yake.
29 Na atie kinywa chake mavumbini;Ikiwa yamkini liko tumaini.
30 Na amwelekezee yule ampigaye shavu lake;Ashibishwe mashutumu.
31 Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtuHata milele.
32 Maana ajapomhuzunisha atamrehemu,Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.