49 Jicho langu latoka machozi lisikome,Wala haliachi;
50 Hata BWANA atakapoangaliaNa kutazama toka mbinguni.
51 Jicho langu lanitia huzuni nafsini mwangu,Kwa sababu ya binti zote za mji wangu.
52 Walio adui zangu bila sababuWameniwinda sana kama ndege;
53 Wameukatilia mbali uhai wangu gerezani,Na kutupa jiwe juu yangu.
54 Maji mengi yalipita juu ya kichwa changu,Nikasema, Nimekatiliwa mbali.
55 Naliliitia jina lako, BWANA, kutoka lile shimoLiendalo chini kabisa.