8 Naam, nikilia na kuomba msaada,Huyapinga maombi yangu.
9 Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa;Ameyapotosha mapito yangu.
10 Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye,Kama simba aliye mafichoni.
11 Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua;Amenifanya ukiwa.
12 Ameupinda upinde wake,Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale.
13 Amenichoma viunoKwa mishale ya podo lake.
14 Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote;Wimbo wao mchana kutwa.