2 Nalikuwa nimelala, lakini moyo wangu u macho,Sikiliza! Mpendwa wangu anabisha!Nifungulie, umbu langu, mpenzi wangu,Hua wangu, mkamilifu wangu,Kwa maana kichwa changu kimelowa umande,Nywele zangu zina manyunyu ya usiku.
3 Nimeivua kanzu yangu; niivaeje?Nimeitawadha miguu; niichafueje?
4 Mpendwa wangu aliutia mkono wake tunduni,Na moyo wangu ukachomeka kwa ajili yake.
5 Nikaondoka nimfungulie mpendwa wangu;Mikono yangu ilidondoza manemane,Na vidole vyangu matone ya manemane,Penye vipini vya komeo.
6 Nalimfungulia mpendwa wangu,Lakini mpendwa wangu amegeuka amepita;(Nimezimia nafsi yangu aliponena),Nikamtafuta, nisimpate,Nikamwita, asiniitikie.
7 Walinzi wazungukao mjini waliniona,Wakanipiga na kunitia jeraha,Walinzi walindao kuta zakeWakaninyang’anya shela yangu.
8 Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu,Ninyi mkimwona mpendwa wangu,Ni nini mtakayomwambia?Ya kwamba nazimia kwa mapenzi.