3 Nimeivua kanzu yangu; niivaeje?Nimeitawadha miguu; niichafueje?
4 Mpendwa wangu aliutia mkono wake tunduni,Na moyo wangu ukachomeka kwa ajili yake.
5 Nikaondoka nimfungulie mpendwa wangu;Mikono yangu ilidondoza manemane,Na vidole vyangu matone ya manemane,Penye vipini vya komeo.
6 Nalimfungulia mpendwa wangu,Lakini mpendwa wangu amegeuka amepita;(Nimezimia nafsi yangu aliponena),Nikamtafuta, nisimpate,Nikamwita, asiniitikie.
7 Walinzi wazungukao mjini waliniona,Wakanipiga na kunitia jeraha,Walinzi walindao kuta zakeWakaninyang’anya shela yangu.
8 Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu,Ninyi mkimwona mpendwa wangu,Ni nini mtakayomwambia?Ya kwamba nazimia kwa mapenzi.
9 Mpendwa wa namna gani ni mpendwa wako,Wewe uliye mzuri katika wanawake,Mpendwa wa namna gani ni mpendwa wako,Hata wewe utusihi hivyo?