46 kutoka huko Ekroni mpaka baharini, yote iliyokuwa upande wa Ashdodi, pamoja na vijiji vyake.
47 Ashdodi, na miji yake na vijiji vyake; na Gaza, na miji yake na vijiji vyake; mpaka kijito cha Misri, na bahari kubwa, na mpaka wake.
48 Na katika nchi ya vilima, Shamiri, na Yatiri, na Soko;
49 na Dana, na Kiriath-sana (ambao ni Debiri);
50 na Anabu, na Eshtemoa, na Animu;
51 na Gosheni, na Holoni, na Gilo; miji kumi na mmoja, pamoja na vijiji vyake.
52 Arabu, na Duma, na Eshani;