17 Kisha kura ya nne ilitokea kwa ajili ya Isakari, maana, ni kwa ajili ya wana wa Isakari kwa kuandama jamaa zao.
18 Na mpaka wao ulifikilia Yezreeli, na Kesulothi, na Shunemu;
19 na Hafaraimu, na Shioni, na Anaharathi;
20 na Rabithu, na Kishioni, na Ebesi;
21 na Remethi, na Enganimu, na Enhada, na Bethpasesi;
22 na mpaka ukafikilia hata Tabori, na Shahasuma na Bethshemeshi; na matokeo ya mpaka wao yalikuwa katika mto wa Yordani; miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
23 Huu ndio urithi wa kabila ya wana wa Isakari kwa kuandama jamaa zao; miji hiyo pamoja na vijiji vyake.