41 Na mpaka wa urithi wao ulikuwa ni Sora, na Eshtaoli, na Irishemeshi;
42 na Shaalabini, na Aiyaloni, na Ithla;
43 na Eloni, na Timna, na Ekroni;
44 na Elteka, na Gibethoni, na Baalathi;
45 na Yehudi, na Bene-beraki, na Gathrimoni;
46 na Meyarkoni, na Rakoni, pamoja na huo mpaka uliokuwa mkabala wa Yafa.
47 Kisha mpaka wa wana wa Dani ulitokea kuwapita wao; kwa kuwa hao wana wa Dani wakakwea na kupigana na Leshemu, na kuutwaa, na kuupiga kwa makali ya upanga, na kuumiliki, nao wakakaa humo, wakauita Dani, kwa kuliandama jina la huyo Dani mzee wao.