1 Siku hiyo, Debora na Baraki, mwana wa Abinoamu, wakaimba wimbo huu:
2 “Viongozi walijitokeza kuongoza Israeli,watu walijitolea kwa hiari yao.Mshukuruni Mwenyezi-Mungu!
3 “Sikilizeni, enyi wafalme!Tegeni sikio, enyi wakuu!Nitamwimbia Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli.
4 “Ee Mwenyezi-Mungu, ulipotoka huko Seiri,ulipoteremka mlimani Edomu,nchi ilitetemeka,mbingu zilidondosha maji,naam, mawingu yakaiangusha mvua.
5 Milima ilitikisika mbele yako Mwenyezi-Mungu,naam, mlima Sinai mbele yako Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli.
6 “Katika siku za Shamgari, mwana wa Anathi,katika wakati wa Yaeli,misafara ilikoma kupita nchini,wasafiri walipitia vichochoroni.