64 Yesu akamwambia, Wewe umesema; lakini nawaambieni, Tangu sasa mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija juu ya mawingu ya mbinguni.
65 Ndipo Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akisema, Amekufuru; mna haja gani tena ya mashahidi? Tazameni, sasa mmesikia hiyo kufuru yake;
66 mwaonaje ninyi? Wakajibu, wakasema, Imempasa kuuawa.
67 Ndipo wakamtemea mate ya uso, wakampiga makonde; wengine wakampiga makofi,
68 wakisema, Ewe Kristo, tufumbulie; ni nani aliyekupiga?
69 Na Petro alikuwa ameketi nje behewani; kijakazi mmoja akamwendea, akasema, Wewe nawe ulikuwapo pamoja na Yesu wa Galilaya.
70 Akakana mbele ya wote, akisema, Sijui usemalo.