15 Akamgusa mkono, homa ikamwacha; naye akaondoka, akawatumikia.
16 Hata kulipokuwa jioni, wakamletea wengi wenye pepo; akawatoa pepo kwa neno lake, akawaponya wote waliokuwa hawawezi,
17 ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema,Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu,Na kuyachukua magonjwa yetu.
18 Naye Yesu alipoona makutano mengi wakimzunguka, aliamuru kuvuka kwenda ng’ambo.
19 Mwandishi mmoja akamwendea, akamwambia, Mwalimu, nitakufuata ko kote uendako.
20 Yesu akamwambia, Mbweha wana pango, na ndege wa angani wana viota; lakini Mwana wa Adamu hana pa kulaza kichwa chake.
21 Mwingine katika wanafunzi wake akamwambia, Bwana, nipe ruhusa kwanza, niende nikamzike baba yangu.