21 Kwa maana alisema moyoni mwake, Nikigusa tu upindo wa vazi lake nitapona.
22 Yesu akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, binti yangu; imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile.
23 Yesu alipofika nyumbani kwa yule jumbe, aliona wapiga filimbi, na makutano wakifanya maombolezo,
24 akawaambia, Ondokeni; kwa maana kijana hakufa, amelala tu. Wakamcheka sana.
25 Lakini makutano walipoondoshwa, aliingia, akamshika mkono; yule kijana akasimama.
26 Zikaenea habari hizi katika nchi ile yote.
27 Yesu alipokuwa akipita kutoka huko, vipofu wawili wakamfuata wakipaza sauti, wakisema, Uturehemu, Mwana wa Daudi.