1 Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia,
2 Tuma watu, ili waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani, niwapayo wana wa Israeli; katika kabila ya baba zao mtamtuma mtu mmoja, kila mtu na awe mkuu kati yao.
3 Basi Musa akawatuma kutoka nyika ya Parani kama alivyoagizwa na BWANA; wote walikuwa ni watu walio vichwa vya wana wa Israeli.
4 Na majina yao ni haya; katika kabila ya Reubeni, Shamua mwana Zakuri.
5 Katika kabila ya Simeoni, Shafati mwana wa Hori.
6 Katika kabila ya Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.
7 Katika kabila ya Isakari, Igali mwana wa Yusufu.