11 Mna ruhusa kula katika nyuni wote walio safi.
12 Lakini hawa msiwale; tai, na furukombe, na kipungu;
13 na kengewa, na kozi, na mwewe kwa aina zake;
14 na kila kunguru kwa aina zake;
15 na mbuni, na kirukanjia, na dudumizi, na kipanga kwa aina zake;
16 na bundi, na mumbi, na bundi mkubwa;
17 na mwari, na nderi, na mnandi;