1 Sikilizeni, enyi mbingu, nami nitanena;Na nchi isikie maneno ya kinywa changu.
2 Mafundisho yangu yatadondoka kama mvua,Maneno yangu yatatona-tona kama umande;Kama manyunyu juu ya majani mabichi;Kama matone ya mvua juu ya mimea.
3 Maana nitalitangaza Jina la BWANA;Mpeni ukuu Mungu wetu.
4 Yeye Mwamba, kazi yake ni kamilifu;Maana, njia zake zote ni haki.Mungu wa uaminifu, asiye na uovu,Yeye ndiye mwenye haki na adili.
5 Wametenda mambo ya uharibifu,Hawawi watoto wake, hii ndiyo ila yao;Wao ni kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka.