1 Hii ndiyo baraka ya Musa, huyo mtu wa Mungu, aliyowabarikia wana wa Israeli kabla ya kufa kwake.
2 Akasema,BWANA alitoka Sinai,Akawaondokea kutoka Seiri;Aliangaza katika kilima cha Parani,Akaja Meribath-kadeshi.Upande wa mkono wake wa kuumePalikuwa na sheria ya moto-moto kwao.
3 Hakika awapenda hayo makabila ya watu;Watakatifu wake wote wamo mkononi mwako;Nao waliketi miguuni pako;Watapokea kila mmoja katika maneno yako.
4 Musa alituagiza torati,Ni urithi kwa mkutano wa Yakobo.