5 Vilindi vimewafunikiza,Walizama vilindini kama jiwe.
6 BWANA, mkono wako wa kuume umepata fahari ya uwezo,BWANA, mkono wako wa kuume wawaseta-seta adui.
7 Kwa wingi wa ukuu wako wawaangusha chini wanaokuondokea,Wapeleka hasira yako, nayo huwateketeza kama mabua makavu.
8 Kwa upepo wa mianzi ya pua yako maji yalipandishwa,Mawimbi yakasimama juu wima mfano wa chungu,Vilindi vikagandamana ndani ya moyo wa bahari.
9 Adui akasema, Nitafuatia, nitapata, nitagawanya nyara,Nafsi yangu itashibishwa na wao;Nitaufuta upanga wangu, mkono wangu utawaangamiza.
10 Ulivuma kwa upepo wako, bahari ikawafunikiza;Wakazama kama risasi ndani ya maji makuu.
11 Ee BWANA, katika miungu ni nani aliye kama wewe?Ni nani aliye kama wewe, mtukufu katika utakatifu,Mwenye kuogopwa katika sifa zako, mfanya maajabu?