17 Ninyi nyote mnaomzunguka, mlilieni,Nanyi nyote mlijuao jina lake, semeni,Jinsi ilivyovunjika fimbo ya enzi,Fimbo ile iliyokuwa nzuri!
18 Ee binti ukaaye Diboni,Shuka toka utukufu wako, ukae katika kiu;Maana atekaye Moabu amepanda juu yako,Ameziharibu ngome zako.
19 Wewe ukaaye Aroeri,Simama kando ya njia upeleleze;Mwulize mwanamume akimbiaye na mwanamke atorokaye,Sema, Imetendeka nini?
20 Moabu ameaibishwa, kwa maana amevunjika;Pigeni yowe na kulia;Tangazeni habari hii katika Arnoni,Ya kuwa Moabu ameharibika.
21 Na hukumu imeifikilia nchi tambarare; juu ya Holoni, na juu ya Yasa, na juu ya Mefaathi;
22 na juu ya Diboni, na juu ya Nebo, na juu ya Beth-diblathaimu;
23 na juu ya Kiriathaimu, na juu ya Beth-gamuli, na juu ya Beth-meoni;