21 Basi miji ya kabila ya wana wa Benyamini kwa kuandama jamaa zao ilikuwa ni Yeriko, na Beth-hogla, na Emek-kesisi,
22 na Bethiaraba, na Semaraimu, na Betheli;
23 na Avimu, na Para, na Ofra;
24 na Kefar-amoni, na Ofni, na Geba; miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake;
25 na Gibeoni, na Rama, na Beerothi;
26 na Mispa, na Kefira, na Moza;
27 na Rekemu, na Irpeeli, na Tarala;