13 Kisha wakawapa wana wa Haruni kuhani Hebroni pamoja na malisho yake, huo mji wa kukimbilia kwa ajili ya mwuaji, na Libna pamoja na malisho yake;
14 na Yatiri pamoja na malisho yake, na Eshtemoa pamoja na malisho yake;
15 na Holoni pamoja na malisho yake, na Debiri pamoja na malisho yake;
16 na Aini pamoja na malisho yake, na Yuta pamoja na malisho yake, na Bethshemeshi pamoja na malisho yake; miji kenda katika kabila hizo mbili.
17 Tena katika kabila ya Benyamini, Gibeoni pamoja na malisho yake, na Geba pamoja na malisho yake;
18 na Anathothi pamoja na malisho yake, na Almoni pamoja na malisho yake; miji minne.
19 Miji yote ya wana wa Haruni, makuhani, ilikuwa ni miji kumi na mitatu, pamoja na malisho yake.