14 Naye BWANA ataonekana juu yao,Na mshale wake utatoka kama umeme;Na Bwana MUNGU ataipiga tarumbeta,Naye atakwenda kwa pepo za kisulisuli za kusini.
15 BWANA wa majeshi atawalinda;Nao watakula na kuyakanyaga mawe ya teo;Nao watakunywa na kufanya kelele kama kwa divai;Nao watajazwa kama mabakuli, kama pembe za madhabahu.
16 Na BWANA, Mungu wao, atawaokoa siku hiyo,Kama kundi la watu wake;Kwa maana watakuwa kama vito vya taji,Vikimeta-meta juu ya nchi yake.
17 Maana wema wake, jinsi ulivyo mwingi!Na uzuri wake, jinsi ulivyo mwingi!Nafaka itawasitawisha vijana wanaume,Na divai mpya vijana wanawake.