29 Mpeni Mwenyezi-Mungu heshima ya utukufu wa jina lake;leteni tambiko na kuingia nyumbani mwake.Mwabuduni Mwenyezi-Mungu patakatifuni pake.
30 Ee dunia yote; tetemeka mbele yake!Ameuweka ulimwengu imara, hautatikisika.
31 Furahini enyi mbingu na dunia!Yaambieni mataifa, “Mwenyezi-Mungu anatawala!”
32 Bahari na ivume, pamoja na vyote vilivyomo!Furahini enyi mashamba na vyote vilivyomo!
33 Ndipo miti yote msituni itaimba kwa furahambele ya Mwenyezi-Mungu anayekujanaam, anayekuja kuihukumu dunia.
34 Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema,kwa maana fadhili zake zadumu milele!
35 Mwambieni Mwenyezi-Mungu:Utuokoe, ee Mungu wa wokovu wetu,utukusanye pamoja na kutuokoa kutoka kwa mataifa,tupate kulisifu jina lako takatifu,kuona fahari juu ya sifa zako.