23 Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria wa kwanza, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, Yakameamu wa nne.
24 Mmoja wa wana wa Uzieli alikuwa Mika. Mmoja wa wazawa wa Mika alikuwa Shamire.
25 Mmoja wa wazawa wa Ishia nduguye Mika alikuwa Zekaria.
26 Wana wa Merari: Mahli, Mushi na Yaazia;
27 wazawa wa Merari kwa mwanawe Yaazia: Shohamu, Zakuri na Ibri.
28 Wana wa Mahli: Eleazari ambaye hakupata mtoto,
29 Kishi ambaye alikuwa na mwana mmoja: Yerameeli.