6 Jeshi la nzige limeivamia nchi yetu;lina nguvu na ni kubwa ajabu;meno yake ni kama ya simba,na magego yake ni kama ya simba jike.
7 Limeiharibu mizabibu yetu,na kuitafuna mitini yetu.Limeyabambua magamba yake na kuyatupa chini,na matawi yake yameachwa meupe.
8 Lieni kama msichana aliyevaa vazi la guniaakiombolezea kifo cha mchumba wake.
9 Sadaka za nafaka na kinywaji zimetoweka nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu.Makuhani, wahudumu wa Mwenyezi-Mungu, wanaomboleza.
10 Mashamba yamebaki matupu;nchi inaomboleza,maana nafaka imeharibiwa,divai imetoweka,mafuta yamekosekana.
11 Ombolezeni enyi wakulima;pigeni yowe enyi watunza mizabibu.Ngano na shayiri zimeharibika,mavuno yote shambani yameangamia.
12 Mizabibu imenyauka;mitini imedhoofika;mikomamanga, mitende na mitofaa imekauka,naam miti yote shambani imekauka.Furaha imetoweka miongoni mwa watu.