32 Siku zile BWANA akaanza kupunguza Israeli. Hazaeli akawapiga mipakani mwote mwa Israeli;
33 kutoka Yordani upande wa mashariki, nchi yote ya Gileadi, na ya Wagadi, na Wareubeni, na Wamanase, kutoka Aroeri iliopo karibu na bonde la Arnoni, yaani, Gileadi, na Bashani.
34 Basi mambo yote ya Yehu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, na ushujaa wake, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?
35 Yehu akalala na babaze; wakamzika katika Samaria. Na Yehoahazi mwanawe akatawala mahali pake.
36 Na muda Yehu aliotawala juu ya Israeli katika Samaria ulikuwa miaka ishirini na minane.