9 Uta wako ukafanywa wazi kabisa;Viapo walivyopewa kabila vilikuwa neno thabiti;Ukaipasua nchi kwa mito.
10 Milima ilikuona, ikaogopa;Gharika ya maji ikapita;Vilindi vikatoa sauti yake,Vikainua juu mikono yake.
11 Jua na mwezi vikasimama makaoni mwao;Mbele ya nuru ya mishale yako ilipotapakaa,Mbele ya mwangaza wa mkuki wako umeremetao.
12 Ulikwenda katikati ya nchi kwa ghadhabu;Ukawapura mataifa kwa hasira.
13 Ukatokea kwa ajili ya wokovu wa watu wako,Kwa ajili ya wokovu wa masihi wako;Ukakiponda kichwa cha nyumba ya waovu,Ukiuweka wazi msingi hata mwambani.
14 Ukakichoma kichwa cha mashujaa wake kwa fimbo zao wenyewe;Wakaja kama kisulisuli ili kunitawanya;Kama wakifurahi kuwameza maskini kwa siri.
15 Ukaikanyaga bahari kwa farasi zako,Chungu ya maji yenye nguvu.