9 Usipande shamba lako la mizabibu aina mbili za mbegu; yasije yakaondolewa matunda yote, mbegu ulizopanda na maongeo ya mizabibu yako.
10 Usilime kwa ng’ombe na punda wakikokota jembe pamoja.
11 Usivae nguo iliyochanganyikana sufu na kitani pamoja.
12 Ujifanyizie vishada katika pembe nne za mavazi yako ya kujifunika.
13 Mtu akitwaa mke, akamwingilia na kumchukia,
14 kisha akamshitaki mambo ya aibu kumzushia jina baya, akasema, Nimemtwaa mwanamke huyu, nami nilipomkaribia sikuona kwake alama za ubikira;
15 ndipo babaye yule kijana na mamaye watakapotwaa alama za yule kijana za ubikira, wawatolee wazee wa mji langoni;