24 Mnyama aliyeumia mapumbu yake, au kusetwa, au kuvunjwa, au kukatwa, msimtolee BWANA; wala msifanye hivi katika nchi yenu.
25 Wala msisongeze chakula cha Mungu wenu katika wanyama hao mmojawapo kitokacho mkononi mwa mgeni; kwa sababu uharibifu wao u ndani yao, wana kilema ndani yao; hawatakubaliwa kwa ajili yenu.
26 Kisha BWANA akanena na Musa, na kumwambia,
27 Hapo ng’ombe, au kondoo, au mbuzi, akizaliwa, atakuwa pamoja na mamaye muda wa siku saba; na siku ya nane na baadaye atakubaliwa kuwa ni sadaka ya kutolewa kwa BWANA kwa njia ya moto.
28 Tena kama ni ng’ombe, au kama ni kondoo, msimchinje huyo na mwanawe wote wawili kwa siku moja.
29 Tena mtakapomchinjia BWANA dhabihu ya shukrani, mtamchinja ili mpate kukubaliwa.
30 Italiwa siku iyo hiyo; msisaze kitu chake hata asubuhi; mimi ndimi BWANA.