15 Mtu mmoja akamkuta, naye alikuwa anazunguka-zunguka katika nyika; yule mtu akamwuliza, akisema, Unatafuta nini?
16 Akasema, Nawatafuta ndugu zangu; tafadhali uniambie mahali wanakochunga.
17 Yule mtu akasema, Wametoka hapa, maana niliwasikia wakisema, Twendeni Dothani. Basi Yusufu akawafuata ndugu zake akawakuta huko Dothani.
18 Wakamwona toka mbali, na kabla hajawakaribia, wakafanya shauri juu yake ili wamwue.
19 Wakasemezana wao kwa wao, Tazama, yule bwana wa ndoto anakuja.
20 Haya, twende, tukamwue na kumtupa katika birika mojawapo, nasi tutasema, Mnyama mkali amemla; kisha tutaona zitakuwaje ndoto zake.
21 Reubeni akasikia akamwokoa katika mikono yao, akasema, Tusimwue.