26 na Moabu atagaa-gaa katika matapiko yake, naye atadhihakiwa. Kwa maana Israeli, je! Hakuwa dhihaka kwako?
27 Alionekana kati ya wevi? Maana kila umtajapo watikisa kichwa chako.
28 Enyi mkaao Moabu, iacheni miji,Enendeni kukaa majabalini;Mkawe kama njiwa afanyaye kioto chakeKatika ubavu wa mdomo wa shimo.
29 Tumesikia habari za kiburi cha Moabu;Ya kuwa ana kiburi kingi;Jeuri yake, na kiburi chake, na majivuno yake,Na jinsi alivyotakabari moyoni mwake.
30 Najua ghadhabu yake, asema BWANA, ya kuwa si kitu; majisifu yake hayakutenda neno lo lote.
31 Kwa sababu hiyo nitampigia yowe Moabu, naam, nitapiga kelele kwa ajili ya Moabu yote; nitawaombolezea watu wa Kir-heresi.
32 Nitakulilia, Ee mzabibu wa Sibma, kwa vilio vipitavyo vilio vya Yazeri; matawi yako yalipita juu ya bahari, yalifika hata bahari ya Yazeri; atekaye nyara ameyaangukia matunda yako ya wakati wa jua, na mavuno yako ya zabibu.