14 na Yatiri pamoja na malisho yake, na Eshtemoa pamoja na malisho yake;
15 na Holoni pamoja na malisho yake, na Debiri pamoja na malisho yake;
16 na Aini pamoja na malisho yake, na Yuta pamoja na malisho yake, na Bethshemeshi pamoja na malisho yake; miji kenda katika kabila hizo mbili.
17 Tena katika kabila ya Benyamini, Gibeoni pamoja na malisho yake, na Geba pamoja na malisho yake;
18 na Anathothi pamoja na malisho yake, na Almoni pamoja na malisho yake; miji minne.
19 Miji yote ya wana wa Haruni, makuhani, ilikuwa ni miji kumi na mitatu, pamoja na malisho yake.
20 Na jamaa za wana wa Kohathi, Walawi, hao wana wengine wa Kohathi waliosalia, wao walikuwa na miji ya kura yao katika kabila ya Efraimu.