3 Maana mataifa yote yalileweshwa kwa divai kali ya uzinzi wake, nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi naye. Nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na anasa zake zisizo na kipimo.”
4 Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema,“Watu wangu, ondokeni kwake,ili msishirikiane naye katika dhambi zake,msije mkaipata adhabu yake.
5 Kwa maana dhambi zake zimekuwa nyingi mno,zimerundikana mpaka mbinguni,na Mungu ameyakumbuka maovu yake.
6 Mtendeeni kama alivyowatendea nyinyi;mlipeni mara mbili kwa yale aliyoyatenda.Mchanganyieni kikombeni mwake kinywaji kikali maradufu.
7 Mpeni mateso na uchungu kadiri ya kujigamba kwake,kulingana na kuishi kwake kwa anasa.Maana anajisemea moyoni: ‘Ninaketi hapa; mimi ni malkia.Mimi si mjane, wala sitapatwa na uchungu!’
8 Kwa sababu hiyo mabaa yake yatampata kwa siku moja:Ugonjwa, huzuni na njaa.Atachomwa moto,maana Bwana Mungu mwenye kumhukumu ana nguvu.”
9 Wafalme wa dunia waliofanya uzinzi naye na kuishi naye maisha ya anasa wataomboleza na kulia wakati watakapoona moshi wa mji huo unaoteketea.