21 Alifuata njia yote aliyoiendea baba yake na kutumikia sanamu ambazo baba yake alizitumikia na kuziabudu.
22 Alimwacha Mwenyezi-Mungu, Mungu wa babu zake, hakushika njia ya Mwenyezi-Mungu.
23 Baadaye watumishi wa Amoni walikula njama na kumwua katika ikulu yake.
24 Lakini watu wa Yuda wakawaua wote waliomuua Amoni. Kisha watu hao wa Yuda wakamtawaza Yosia mwanawe mahali pake.
25 Matendo mengine yote ya Amoni yameandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Yuda.
26 Amoni alizikwa kaburini katika bustani ya Uza; na Yosia mwanawe akatawala mahali pake.