11 Ikiwa Mwenyezi-Mungu ajua yaliyo Kuzimu na Abadoni,mawazo ya binadamu yatawezaje kujificha mbele yake?
12 Mwenye madharau hapendi kuonywa,hatafuti kamwe maoni ya wenye busara.
13 Moyo wa furaha hungarisha uso,lakini uchungu huvunja moyo.
14 Mwenye busara hutafuta maarifa,lakini wapumbavu hujilisha upuuzi.
15 Kwa mnyonge kila siku ni mbaya,lakini kwa mwenye moyo mchangamfu ni sikukuu.
16 Afadhali kuwa na kidogo na kumcha Mwenyezi-Mungu,kuliko kuwa na mali nyingi pamoja na taabu.
17 Afadhali mlo wa jioni wa mchicha na upendo,kuliko karamu ya nyama nono pamoja na chuki.