7 Huwawekea wanyofu akiba ya hekima safi,yeye ni ngao kwa watu waishio kwa uaminifu.
8 Huilinda mienendo ya watu watendao haki,na kuzihifadhi njia za waaminifu wake.
9 Ukinisikiliza utafahamu uadilifu na haki,utajua jambo lililo sawa na jema.
10 Maana hekima itaingia moyoni mwako,na maarifa yataipendeza nafsi yako.
11 Busara itakulinda,ufahamu utakuhifadhi;
12 vitakuepusha na njia ya uovu,na watu wa maneno mapotovu;
13 watu waziachao njia nyofu,ili kuziendea njia za giza;