9 Ukinisikiliza utafahamu uadilifu na haki,utajua jambo lililo sawa na jema.
10 Maana hekima itaingia moyoni mwako,na maarifa yataipendeza nafsi yako.
11 Busara itakulinda,ufahamu utakuhifadhi;
12 vitakuepusha na njia ya uovu,na watu wa maneno mapotovu;
13 watu waziachao njia nyofu,ili kuziendea njia za giza;
14 watu wafurahiao kutenda maovu,na kupendezwa na upotovu wa maovu;
15 watu ambao mienendo yao imepotoka,nazo njia zao haziaminiki.