1 Anayeonywa mara nyingi akawa mkaidi,ataangamia ghafla asipone tena.
2 Waadilifu wakitawala watu hufurahi,lakini waovu wakitawala watu hulalamika.
3 Apendaye hekima humfurahisha baba yake;lakini aandamanaye na malaya hufuja mali yake.
4 Mfalme akitumia haki huipatia nchi uthabiti,lakini akipenda hongo taifa huangamia.