9 Mwenye hekima akibishana na mpumbavu,mpumbavu huwaka hasira na kucheka bila kutulia.
10 Wapendao kumwaga damu humchukia mtu asiye na hatia,lakini watu wema huyalinda maisha yake.
11 Mpumbavu huonesha hasira yake wazi,lakini mwenye hekima huizuia na kuituliza.
12 Mtawala akisikiliza mambo ya uongo,maofisa wake wote watakuwa waovu.
13 Maskini na mkandamizaji wanafanana kwa kitu kimoja:Wote wawili wamepewa macho na Mwenyezi-Mungu.
14 Mfalme anayewaamua maskini kwa haki,atauona utawala wake umeimarika milele.
15 Adhabu na maonyo huleta hekima,lakini mtoto aliyeachwa afanye apendavyo humwaibisha mama yake.