11 Mwanangu, usidharau adhabu ya Mwenyezi-Mungu,wala usiudhike kwa maonyo yake;
12 maana Mwenyezi-Mungu humwonya yule ampendaye,kama baba amwonyavyo mwanawe mpenzi.
13 Heri mtu anayegundua hekima,mtu yule anayepata ufahamu.
14 Hekima ni bora kuliko fedha,ina faida kuliko dhahabu.
15 Hekima ina thamani kuliko johari,hamna unachotamani kiwezacho kulingana nayo.
16 Kwa mkono wake wa kulia Hekima atakupa maisha marefu;kwa mkono wake wa kushoto atakupa mali na heshima.
17 Njia zake ni za kupendeza,zote zaelekea kwenye amani.