22 navyo vitakuwa uhai nafsini mwako,na pambo zuri shingoni mwako.
23 Hapo utaweza kwenda zako kwa usalama,wala mguu wako hautajikwaa.
24 Ukiketi hutakuwa na hofu;ukilala utapata usingizi mtamu.
25 Usiogope juu ya tishio la ghafla,wala shambulio kutoka kwa waovu,
26 Maana Mwenyezi-Mungu ndiye atakayekutegemeza;atakuepusha usije ukanaswa mtegoni.
27 Usimnyime mtu anayehitaji msaada,ikiwa unao uwezo wa kufanya hivyo.
28 Usimwambie jirani yako aende zake hadi kesho,hali wewe waweza kumpa anachohitaji leo.