13 Hutafuta sufu na kitani,na kufanya kazi kwa mikono yake kwa bidii.
14 Yeye ni kama meli za biashara:Huleta chakula chake kutoka mbali.
15 Huamka kabla ya mapambazuko,akaitayarishia jamaa yake chakula,na kuwagawia kazi watumishi wake.
16 Hufikiria kununua shamba, kisha hulinunua,na kulima zabibu kwa faida ya jasho lake.
17 Huwa tayari kufanya kazi kwa nguvuna kuiimarisha mikono yake.
18 Hutambua kwamba shughuli zake zina faida;hufanya kazi hata usiku kwa mwanga wa taa yake.
19 Husokota nyuzi kwa mikono yake mwenyewe,kwa vidole vyake mwenyewe husuka nguo zake.