2 umejibana kwa maneno yako mwenyewe,umejinasa kwa ahadi uliyofanya.
3 Ujue kwamba uko chini ya mamlaka ya mwenzio,lakini mwanangu, ukitaka kujiokoa, basi fanya hivi:Mwendee mtu huyo mara moja umsihi akupe uhuru wako.
4 Jitahidi usiache macho yako yapate usingizi,wala kope za macho yako zisinzie.
5 Jiokoe kwa kujitoa katika mtego huo,mithili ya paa ama ndege amtorokavyo mwindaji.
6 Ewe mvivu! Hebu ukamchungulie sisimizi,fikiria namna yake ya kuishi ukapate hekima.
7 Sisimizi hana kiongozi, ofisa, wala mtawala;
8 lakini hujiwekea chakula wakati wa kiangazi,hujikusanyia akiba wakati wa mavuno.